Follow this blog with bloglovin

Ads

Vikeki Vya Icing Za Rangi




Vipimo



Unga                                              1 ½ Vikombe

Baking powder                                1 Kijiko cha chai

Chumvi                                           ½ Kijiko cha chai

Siagi isiyo na chumvi                        ½ Kikombe

Sukari                                              1 Kikombe

Mayai                                               3

Vanilla                                              1½ Vijiko vya chai

Maziwa                                             ¾ Kikombe




Namna Ya Kutayarisha Na Kupika



  1. Washa oveni moto wa 350°. Kisha weka karatasi za kupikia keki za vikombe kwenye treya.
  2. Katika bakuli la kiasi, chunga pamoja unga, baking powder na chumvi na iache kando.
  3. Katika bakuli la mashine changanya siagi na sukari hadi ilainike.
  4. Halafu tia yai moja baada la jengine huku unaendelea kuchanganya, kisha tia vanilla.
  5. Kisha tia mchanganyiko wa unga uliyoweka kando nusu yake huku unaendelea kuchanganya, kisha tia maziwa na umalizie na unga uliyobakia.
  6. kisha mimina kwenye treya/karatasi za kuchomea keki za vikombe lakini usijaze mpaka juu.
  7. Weka katika oveni kwa muda wa dakika 20.
  8. Ziache zipoe kisha zipake icing/cream upendayo na zitakuwa tayari kuliwa.

Kidokezo

Kipimo hichi ni ya vikeki darzeni moja.
SHARE

Author

Hi, Its me Hafeez. A webdesigner, blogspot developer and UI/UX Designer. I am a certified Themeforest top Author and Front-End Developer. I'am business speaker, marketer, Blogger and Javascript Programmer.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: