Follow this blog with bloglovin

Ads

PILAU YA KUKU (YA KUPIKA NA RICE COOKER)

Moja kati ya njia ninayoonaa ni rahisi na ya haraka kupika pilau ni kutumia rice cooker , leo nitaelezea jinsi ya kuipika na njia zinazofanya iwe rahisi zaidi.  
MAHITAJI 
Mchele nusu kg 
Kuku mlaini nusu kg
Viazi mviringo  (mbatata) 2 vimenye na vikate
Kitunguu saum  kijiko 1 cha supu (garlic)
Tangawizi mbichi kijiko 1 cha supu(ginger)
Bizari nyembamba  (uzile) kijiko 1 cha supu (cumin)
Mdalasini vipande 3 vya kiasi au kijiko 1 cha aupu(cinnamon)
Pilipili manga kijiko 1 cha chai (black pepper )
Kidonge cha supu cha kuku 1 (chicken maggi)
Garam masala kijiko 1 cha chai  (sio lazima)
Iliki chembe 4(cardamom)
Karafuu kava chembe 4(dried cloves)
Vitunguu maji kilichokaangwa kikombe 1 (nimetumia vitunguu maji vya kunnua, vipo tayari kupikia ) (onion)
Keroti  (carrot ) 1 , imenye na ikate ndogo ndogo 
Mafuta ya kupikia robo kikombe  (yakihitajika) (cooking oil)
Chumvi (salt)
Spaisi zote zikiwa za unga ni vizuri zaidi, 
Kwenye rice cooker, tia kuku uliekwisha mtengeneza na kumkosha vizuri ,chumvi, kitunguu saum, tangawizi, viazi , carrot, kidonge cha supu na spaisi zote 
Tia maji vikombe 3 au zaidi, inategemea na supu unayotaka kulingana na mchele wako, 
Funika ,washa rice cooker ,kuku achemke awive pamoja na viazi na ibaki na supu kiasi
Tia vitunguu maji , mchele na mafuta yakihitajika, kama kuku atakua na mafuta ya kutosha usitie mafuta, koroga kidogo funika wacha mpaka wali uwive ,ukauke ,funua uchanganye na pilau itakua tayari kuliwa.
●Kipimo cha supu inategemea na mchele utakaotumia au unaweza kutumia kipimo cha kikombe cha rice cooker, 
●Mara nyingi nakua nakisia maji au supu au nikitumia kipimo cha rice cooker naengeza kama kama nusu kikombe.
●unaweza kuengeza kiasi cha spaisi kama unataka pilau ikolee rangi.
●unapotumia kuku mlaini ndio unazidi kua rahisi sababu unatumia rice cooker kupikia na anawiva haraka. 
●unaweza kukaanga vitunguu mwenyewe vingi ukaweka kwenye fridge au freezer na kutumia unapovihitaji au unaweza kununua dukani vilivyokua tayari kutumia/vilivyokwisha kaangwa  (fried onions ).
VITUNGUU VILIVYOKWISHA KAANGWA
MUONEKANO WA VITUNGUU VYA KUNUNUA VILIVYOKAANGWA .
BAADHI YA HATUA UNAZOPITIA UNAPOPIKA PILAU KWENYE RICE COOKER 
SHARE

Author

Hi, Its me Hafeez. A webdesigner, blogspot developer and UI/UX Designer. I am a certified Themeforest top Author and Front-End Developer. I'am business speaker, marketer, Blogger and Javascript Programmer.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: