Follow this blog with bloglovin

Ads

FAIDA ZINAZO PATIKANA KATIKA KUWAAMINI MALAIKA

  1. Tunapaswaa kujua utukufu wa mwenyezi mungu mtukufu na uwezo wake na kwamba kakizunguka kila kitukwa elimu yake, maana utukufu wa viumbe ni dalili ya utukufu wa aliye viumba
  2. Kuwaamini malaika kunatuhamasisha katika kufanya yaliyo mema na kutengana na mabaya, kataka hali ya siri na uwazi,pindi pale muislamu anapotambua kuwa kuna malaika wanao sajili maneno yake na vitendo vyake, na kwamba kila alifanyalo litakuwa ima la kheri au la shari.
  3. Kuwaamini malaika kunatusaidia kutengana na mambo ya uzushi, na itikadi batili walizonazo wasio amini ghaibu(mambo yasiyo onekana).
  4. Tunapata kujua huruma ya mwenyezi mungu kwa waja wake, kwa kule kuwaekea malaika wanao wahifadhi na kuyaendesha mambo yao.
  5. Kuviamini vitabu,Ni kuamini mwenyezi mungu mtukufu, kateremsha vitabu kutoka kwake,kaviteremsha kwa mitume wake,ili wavifikishe kwa watu, na kwamba vitabu hivyo vimebeba haki, na kumpwekesha mwenyezi mungu katika uungu wake na uumbaji wake na katika majina na sifa zake. Amesema mwenyezi mungu mtukufu;"kwa hakika tuliwapeleka mitume mitume wetu kwa dalili za waziwazi na tukaviteremsha vitabu na uadilifu pamoja nao, ili watu wasimamie uadilifu"Al- hadyd;25, Na mwislamu anatakiwa kuviamini vitabu vyote vilivyo teremshwa kabla ya qur-ani, na kuamini kuwa vinatoka kwa mwenyezi mungu, lakini hawajibiki kuvifanyia kazi na kuvifuata bada ya kushuka qur-ani, kwa sababu vitabu hivyo vimeteremsha kwa muda maalumu na kwa watu maalumu. miongoni mwa vitabu hivyo ambavyo mwenyezi mungu kavielekeza ni:
  • Swahifu za ibhrahimu na musa
  • Taurati
  • Zaburi
  • Injili
  • Qur-ani tukufu
           Ni wajibu kuamini kuwa ni maneno ya mwenyezi mungu, ambayo kashuka nayo malaika Jibrilu kwa mtume muhammad Rehma na amani za allah ziwe juu yake yakiwa katika lugha ya kiarabu iliyo fasaha. Amesema mwenyezi mungu mtukufu;"Amemteremsha roho muaminifu,(Jibril). Juu ya moyo wako ili uwe miongini mwa waonyaji. kwa lugha ya kiarabu waziwazi(fasihi)"Ash-shu`araa:193-195

                                                                                                               imechapishwa na:
                                                                                                                                             shafii bin omary

SHARE

Author

Hi, Its me Hafeez. A webdesigner, blogspot developer and UI/UX Designer. I am a certified Themeforest top Author and Front-End Developer. I'am business speaker, marketer, Blogger and Javascript Programmer.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: