Follow this blog with bloglovin

Ads

CHAI YA MASALA/MASALA TEA


Chai ya masala ni chai ya viungo  (spices) ambayo unaweza kuipika vile unavyopenda, aidha ya maziwa au kavu, nikija upande wangu mimi napenda sana chai kavu, ila nikitamani chai ya maziwa lazima iwe ya masala , 
MAHITAJI 
Maziwa ya maji lita 1
Majani ya chai pakti 2 au vijiko 2 vya supu 
Zaatari kijiko 1 cha chai 
Iliki chembe 3
Karafuu kavu chembe 3
Mdalasini kipande 1 cha kiasi 
Tangawizi mbichi au kavu kiasi unachopenda 
Sukari
Weka vitu vyote kwenye sufuria isipokua tangawizi na sukari  , unaweza kuengeza na maji au ukawacha maziwa matupu, 
Iweke kwenye moto wacha ichemke vizuri, 
Ikichemka vizuri kama imefanya mapovu juu ikoroge yale mapovu yaondoke, 
Hakikisha imeshachemka vizuri kwa dakika angalau 2 , saga tangawizi na utie kwenye chai, moto usiwe mdogo maziwa yanaweza kukatika , wacha ichemke tena kwa dakika 1 na epua , ichuje na Iweke/itie kwenye chupa au vikombe.


  • Unaweza kuweka sukari kabisa au unaweza kukorogea kwenye kikombe 
  • Ili maziwa yasikatike  hakikisha chai imechemka vizuri kabla kuweka tangawizi, AU yachemshe maziwa pekee kwanza mpaka yachemke vizuri ndio utie vitu viliobaki
  • Sufuria ya kupikia chai isiwe unapikia vyakula vyengine , bila hivo inaweza kusababisha chai/maziwa yakatike 
  • Ukipenda unaweza kutia mchaichai na pilipili manga, inazidi kua tamu.  
SHARE

Author

Hi, Its me Hafeez. A webdesigner, blogspot developer and UI/UX Designer. I am a certified Themeforest top Author and Front-End Developer. I'am business speaker, marketer, Blogger and Javascript Programmer.

  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
  • Image
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments: